Image
Image

EMANUELI OKWI SASA KUMPIGA NGWALA MOSES OLOYA WA UGANDA.


Msuguano mkali wa kumnasa kiungo nyota mshambuliaji wa uganda, moses oloya inazidi kushika kasi na sasa simba imeamua kufanya fitna kwa kumtumia mshambuliaji wake wa zamani, emmanuel okwi amalize mchezo.

Simba ndiyo ilikuwa ya kwanza kumwania oloya anayekipiga katika kikosi cha klabu ya saigon xuan thanh ya vietnam, lakini yanga nao 'wakatia mguu'.

kwa kuwa yanga waliamua kuingia na kuanza kazi ya kumnasa oloya likiwa ni ombi la kocha wao, ernie brandts, aliyesisitiza anamhitaji mganda huyo, simba wameamua kumtumia okwi ambaye pia amemsisitiza oloya kuwa sehemu sahihi ni simba.

chanzo cha uhakika kimeeleza, simba ilimtuma geofrey nyange 'kaburu' kwenda uganda ambako alifanya mazungumzo na oloya kwa mara nyingine akiwa katika kambi ya the cranes.

"kaburu ambaye alikwenda kwa niaba ya (zacharia) hans pope ambaye mwanzo ndiye alizungumza na oloya. pia alimtumia okwi amshawishi oloya kuhusiana na simba na maisha yake yalivyo, najua atakuwa amemueleza yanga hakumfai.


"kweli okwi alifanya naye mazungumzo na kumsisitiza kama anataka kuja tanzania, basi timu sahihi ni simba. kwangu sidhani kama kweli oloya anaweza kubadilika maana ni rafiki wa karibu wa okwi," kilieleza chanzo hicho cha uhakika.

"okwi na oloya wanaelewana sana, wamekuwa marafiki kwa kipindi kirefu. hivyo dalili zote zinaonyesha kuwa oloya atatua simba."

yanga ilifanya juhudi hadi kumtuma mwakilishi nchini vietnam kuhakikisha inamnasa, lakini viongozi wake walikanusha baada ya kuona mpango umejulikana na oloya aliwataka watoe dola 100,000 (zaidi ya sh milioni 160) kama alivyokuwa amewaeleza simba.

kuona hivyo, simba wakaongeza nguvu kwa hofu ya kumkosa. timu hizo zinalazimika kusubiri mkataba wake umalizike ili atue nchini na kila upande bado unamhitaji. taarifa zinadai nyota huyo atatua nchini agosti 28, mwaka huu.

 source: Championi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment