Image
Image

JUMAZA YALAANI KITENDO CHA KUMWAGIWA TINDIKALI RAIA WA UINGEREZA KATIKA ENEO LA MJI MKONGWE ZANZIBAR HIVI KARIBUN.





Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAZA)   imelaani vikali  kitendo cha  kumwagiwa maji yanayosadikiwa kuwa ni tindi kali raiya wawili wa kike wa Uingereza katika eneo la Mji Mkongwe wa Zanzibar hivi karibuni.
Tamko hilo limetolewa na Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo Muhidin Zubeir Muhidini  katika ukumbi wa hoteli ya Mazson’s wakati alipokuwa  akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo.
Muhiddin alisema  kitendo cha kumwagiwa tindikali raia hao Kirstie Trup na Katie Gee  kina lengo la  kuitia doa   Zanzibar ambayo inasifika kuwa  ni  kisiwa cha  amani  na ukarimu wa kuwapokea vizuri wageni.Aliwataka wazanzibari kuendeleza ukarimu kwa wageni na kudumisha  amani na utulivu, na kutotoa mwanya kwa watu au vikundi vya watu vyenye nia mbaya ya kutaka kusababisha mizozo kwa malengo yao binafsi na kuiharibu heshima ya Zanzibar.
Katibu huyo aliliomba Jeshi la Polisi nchini kufanya uchunguzi wa kina  na waharaka ili kubaini wahusika wa tukio hilo na kuwafikisha katika   vyombo vya  sheria .

Aidha aliliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa  tukio hilo  kwa uadilifu bila ya kupokea shinikizo kutoka sehemu yoyote  ili  ukweli upatikane bila ya kuwadhuru  watu wasiohisika na tukio hilo .
Sambamba na  tukio hilo JUMAZA imeshtushwa na tukio la kupigwa risasi  Mhadhiri  wa dini ya kiislam Sheikh Issa  Ponda  huko Morogoro katika mazingira ambayo hadi sasa yanaonekana kuwa na utata. .
Aidha alikemea vikali kauli ya baadhi ya vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi , ambavyo vinahusisha matukio ya aina hiyo na waumini wa dini ya Kiislamu.
Amesema  vyombo vya habari vinawajibu wa kutoa habari zilizo fanyiwa utafiti wa kina na kuacha tabia ya  kukurupuka  kwa lengo la kutafuta umaarufu, huku wakiliacha Taifa kwenye  machafuko kama tunavyoshuhudia baadhi ya nchi  ulimwenguni.
“Vyombo vya habari visiwe chanzo cha  machafuko kwa kutoa taarifa zisizofanyiwa uchunguzi na hatimae kusababisha machafuko,“ alisisitiza Katibu Mtendaji wa JUMAZA..
Ameitaka Jamii ya  Kimataifa  kwa upande wake kuwa  waangalifu na taarifa zinazotolewa na baadhi ya vyombo vya habari ambavyo lengo lake ni kuichafua  Zanzibar kimataifa.

Zanzibar yaleo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment