Image
Image

Ndalichako awa Rais Mabaraza ya Mitihani Afrika


                   Dk. Joyce Ndalichako
Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), Dk. Joyce Ndalichako amechaguliwa kuwa Rais wa  Mabaraza ya Mitihani Barani Afrika (AEAA ) kwa kipindi cha mwaka mmoja.



Ndalichako alichaguliwa kushika wadhifa huo uliokuwa ukishikiliwa na Raia wa Kenya, aPaulo Wasanga katika  mkutano uliofanyika jijini hapa wa masuala ya elimu, ambao uliwakutanisha wadau wa elimu kutoka nchi zaidi ya 20 za Bara la Afrika.



Baada ya kuchaguliwa,  Ndalichako alisema cheo hicho ni heshima kwa nchi ya Tanzania na Watanzania kwa ujumla na kuwaomba wadau wa elimu kushirikiana naye kuleta mabadiliko makubwa ya elimu nchini.



Alisema katika kipindi atakachoongoza mabaraza hayo, atahakikisha anaboresha maendeleo kwa kila nchi hususan Tanzania na kusisitiza kuwa ushirikiano katika utendaji wa kazi ni muhimu ili kuinua sekta ya elimu kwa nchi hizo.



Ndalichako alisema  ili kufikia lengo la ufaulu ni lazima kutoa nafasi kwa watumishi  wa mabaraza ya mitihani wajifunze mbinu  za ufaulu.



Akizungumzia kuhusu mkutano huo, alisema umewezesha wadau wa mabaraza ya mitihani kutoka bara hilo  kutathimini usahihishaji wa  mitihani na kuweza kutumia kompyuta kwa ajili ya kuchagua majibu sahihi ya mitihani.



Ndalichako aliiomba serikali kushirikiana naye ili kuwezesha sekta ya elimu kukua.

Nipashe.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment