Image
Image

VIONGOZI WANNE WA DECI WAHUKUMIWA JELA MIAKA MITATU KATIKA MAHAKAMA HAKIMU MKAZI KISUTU JIJINI DAR ES SALAAM



Salum mkambala, Dar es Salaam

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam  imewahukumu pasipo shaka,miaka mitatu jela au kulipa adhabu ya shilingi milioni 21kila mmoja viongozi wanne wa kampuni ya Kusimamia na Kuendesha Upatu (DECI) na kumuachia huru mshtakiwa wa tano baada ya washtakiwa hao wanne kupatikana na hatia katika mashtaka yote mawili ya kuendesha shughuli hizo kinyume cha sheria.

Washtakiwa hao ni Jackson Mtares, Dominic Kigendi, Samuel Mtares, Timotheo ole Loitingye na mshtkaiwa wa tano aliachiwa huru baada ya ushahidi katika shauri hilo kutomtia hatiani pasipo shaka ni Arbogast Francis Kipilimba ambapo jumla ya mashahidi 16 wa upande wa mashtaka walitoa ushahidi wao.

Katika mashataka yao walidaiwa kuendesha na kusimamia shughuli za upatu kinyume na sheria na kukusanya amana kutoka kwa umma bila ya kuwa na leseni ambapo wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya mwaka 2007 na Machi 2009 katika Makao Makuu ya DECI, Mabibo, Dar es Salaam.

Akitoa hukumu mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo Aloyce Katemana katika shtaka la kwanza amewataka washtakiwa hao kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya sh.milioni tatu kila mmoja na katika shtaka la pili amewahukumu kila mmoja kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya sh.milioni 18 kila mmoja huku ikitoa amri na maelekezo kwa serikali kupitia benki kuu,BOT kwamba,akaunti  tano zilizokuwa na takribani bilion i,16,viwanja ,nyumba na magari viuzwe na fedha zirudishwe kwa wanachama wa DECI.

 Aidha hadi hadi Tambarare Halisi  inaondoka mahakamani hapo waliofanikiwa kulipa faini hiyo mahakamani hapo na kuwa huru ni,Jackson Mtares na Timotheo ole Loitingye ambapo baadhi ya wanachama wa DECI na wakili aliyekuwa anawatetea washtakiwa hao HUDSON NDUSYEPO wamezungumzia hukumu hiyo.




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment