Image
Image

WANAHARAKATI WAKAMILISHA MATEMBEZI YA KUPINGA UWINDAJI HARAMU NCHINI TANZANIA.



Dar es Salaam.

Kundi la wanaharakati wa kulinda wanyama pori wamekamilisha matembezi ya kilomita 650 kutoka Arusha kwenda mjini Dar es Salaam.

Wanaharakati hao waliandaa matembezi hayo kulalamikia visa vya uwindaji haramu wa ndovu na vifaru. 

Matembezi hayo kwa jina "Walk for the Elephant" yalidhaminiwa na shirika la African Wildlife Trust (AWT) na yalilenga kuhamasisha watu kuhusu athari za uwindaji haramu barani afrika. 

Naibu waziri wa mali asili na utalii wa Tanzania Lazaro Nyalandu anasema ndovu 30, 000 waliuwawa kwa ajili ya pembe zao barani Afrika mwaka jana na nchini Tanzania pekee kila siku ndovu 30 huuwawa.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment