Bingwa wa WBC na WBA wa uzito wa welterweight Floyd Mayweather amesema
anatarajia pambano lake na Manny Pacquiao litafanyika, lakini
makubaliano bado hayajafikiwa.
Mayweather Mmarekani mwenye miaka 37 na
Pacquiao miaka 36 hivi karibuni walipena namba za simu katika mechi ya
mpira wa kikapu, wawili hao wanazingatiwa kuwa mabondia wazuri sana wa
sasa.
Mayweather alisema kumekuwa na uvumi na uzushi mwingi lakini bado
hajasaini makubaliano ila ana imani kubwa kufanyika kwa pambano.
Hivi
karibuni msemaji wa Pacquiao alisema pambano la mabondia hao bado lina
safari ndefu sana lakini kuna matumaini kwamba huenda likafanyika. Hayo
yote yamekuja baada ya ripoti kusema Pacquiao amekubali kupigana na
kwamba pambano litafanyika Mei 2 huko Las Vegas.
0 comments:
Post a Comment