Chama cha wananchi CUF kimeahirisha maandamano yake ambayo yalikuwa wayafanywe na jumuia ya vijana ya chama hicho leo jijini Dar es salaam yakiwa na madhumuni ya kushinikiza tume ya uchaguzi kuongeza siku za kuandikisha wapiga kura.Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Prof.Ibrahim lipumba amesema kwamba kuahirishwa kwa maandamano hayo tayari wameshalipa taarifa Jeshi la Polisi kupitia Kamanda wa kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova.
Kabla ya kuahirishwa maandamano hayo tayari Jeshi la Polisi lilipiga marufuku maandamano ya Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Wananchi CUF yaliyotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam leo.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment