Mshambuliaji staa wa timu ya Chelsea, Didier Drogba ameamua kujenga
zahanati ya kwanza katika Jiji la Abijan, Ivory Coast kwa lengo la
kusaidia jamii yake chini ya Mfuko wa Didier Drogba.
Hii ni ya kwanza
kati ya tano ambazo Secretary wa Mfuko, Guy Roland Tanoh alizoahidi
kwamba wamejipanga kuzijenga ndani ya Ivory Coast kwa ajili ya kusogeza
huduma hiyo kwa watu Nahodha huyo wa zamani wa timu ya Ivory Coast, hivi
karibuni alitumia ukurasa wake wa Instagram kueleza taarifa hiyo pamoja
na kuweka picha za maendeleo ya ujenzi wa zahanati hiyo ambao
unakaribia kukamilika.
Roland alisema Didier aliona ni bora kujenga
zahanati hizo tano nyumbani kwao kuliko kujenga hospitali moja kubwa kwa
kuwa hospitali moja isingeweza kuhudumia maeneo mbalimbali na kwa wingi
kama ambavyo zahanati zinaweza kuhudumia watu hao.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment