Image
Image

Francis cheka (SMG) atupwa jela miaka mitatu baada ya kukutwa na hatia mahakama ya hakimu mkazi morogoro.



Bondia wa ngumi za kulipwa Tanzania, anayeshikilia mikanda lukuki ikiwemo wa WBF, Francis Cheka, amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu, sambamba na kutakiwa kulipa shilingi milioni moja kama gharama za matibabu na fidia, baada ya kupatikana na hatia ya shambulio la kudhuru mwili dhidi ya meneja wa baa yake ya vijana social, bahati kabanda,mkazi wa morogoro.

 Hukumu hiyo imetolewa na hakimu mkazi mwandamizi katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa morogoro, said msuya, baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na mashahidi wanne wa upande wa mashtaka, ambapo bila shaka umemtia hatiani mshtakiwa kama alivyokuwa akishtakiwa ambapo hakimu msuya amedai kutoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa mshtakiwa na wegine wanaojichukulia sheria mikononi..

Awali imedaiwa na mwendesha mashtaka atuganile msyani kuwa, mshtakiwa ametenda kosa hilo mnamo julai 02 mwaka jana, huko maeneo ya sabasaba manispaa ya morogoro, ambapo bila halali na akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria, alimpiga kwa ngumi maeneo ya kichwani na tumboni,bahati kabanda maarufu kama masika,aliyekuwa meneja wa baa yake ya vijana social, na kumsababishia maumivu makali,tukio linalodaiwa kufanywa  baada ya  cheka kudaiwa kutoridhishwa na mahesabu ya mauzo.

 Hata hivyo alipopewa fursa ya kujitetea na mahakama, cheka alishindwa kufanya hivyo na badala yake kuieleza mahakama kufanya kile itakachokuwa imeamua,na hakimu kumpa adhabu hiyo ya miaka mitatu jela na akimaliza kifungo alipe fidia ya shilingi milioni moja kama fidia na malipo ya gharama za matibabu kwa mlalamikaji, kabanda,hukumu ambayo imezungumziwa na kocha wa cheka saleh komando na mdogo wake cheka ambaye pia ni bondia cosmas cheka.

Hata hivyo, baada ya hukumu hiyo, Cheka alidai kwamba sababu halisi ya kifungo ni fitina za viongozi wa mkoa wa Morogoro baada ya kudai zawadi yake aliyoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete ya bati.
Cheka aliwaambia Waandishi wa Habari
akiwa kwenye gari la Polisi tayari kupelekwa gerezani kwamba, kilichomponza hadi kufungwa leo ni kudai bati alizoahidiwa na Rais Kikwete. 
Kwa ufupi hadi hukumu hii ya cheka july 5  ndio jeshi la polisi moro lilimshikilia soma.
Tarehe 5 July 2014 Jeshi la Polisi mkoani Morogoro lilimshilikia bingwa wa ngumi za kulipwa duniani, Francis Cheka ‘SMG’ kwa tuhuma za kumchapa Meneja wa baa ya Vijana Social Hall iliyopo Kata ya Sabasaba, Manispaa ya Morogoro.

Kwa mujibu wa maelezo ya meneja huyo, Bahati Kabanda ‘Masika’ (39), Cheka alifika katika baa hiyo majira ya jioni na kuanza kumtukana na kumshambulia kwa maneno machafu kisha kumvamia na kuanza kumchapa ngumi na mateke sehemu za tumboni.

Baa hiyo iilikuwa inamilikiwa na promota wa ngumi za kulipwa mkoani Morogoro, Zumo Makame.

Kabanda alidai wakati akipewa kichapo na Cheka, hakuna mtu aliyesogea kuamulia ugomvi huo kutokana na watu kumuogopa bondia huyo aliyewahi kuwapiga mabondia wa ndani na nje ya nchi.

Alidai Cheka alifika katika baa hiyo na dalili za kulewa pombe na baada ya kuondoka, wasamaria wema walimchukua yeye hadi katika hospitali ya rufaa ambako alilazwa na kupatiwa vipimo na matibabu ya maumivu aliyoyapata.

Kabanda alidai kuwa hakuwa na ugomvi na bondia huyo, na hivyo hajui chanzo cha kupigwa na kuongeza kuwa kama alikuwa na ugomvi nae angemfikisha kwenye vyombo vya sheria na sio kujichukulia sheria mkononi.

Masika alidai kuwa pamoja na kupatiwa matibabu, lakini bado hali yake kiafya sio nzuri kutokana na maumivu aliyoyapata ya mbavu, hivyo kumfanya ashindwe kutembea vizuri.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa walimuona Cheka akimuangushia kipigo meneja huyo, lakini walishindwa kuamulia ugomvi huo kutokana na kumwogopa Cheka ambaye ni bingwa wa ngumi duniani.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro, Ritha Lyamuya, alikiri kumpokea Masika hospitalini hapo Juni 2, akiwa na maumivu ya mbavu na walipompima X-ray ilionekana amepata maumivu, hivyo walimpatia matibabu na kumruhusu kurudi nyumbani.

Alisema hadi anaruhusiwa hospitalini hapo, Masika alikuwa anaendelea vizuri.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Leonard Paulo, amekiri Cheka kufanya shambulio hilo kwa meneja huyo kwa kumpiga sehemu za tumboni na kichwani.

Paulo alisema Cheka amekamatwa na anashikiliwa na polisi kwa mahojiano na kwamba katika maelezo yake, anadai kuwa yeye na Masika walikodi baa hiyo na kufanya biashara kwa pamoja, lakini baadaye walianza kukosana katika suala na mapato.

Cheka aliendelea kudai kuwa siku ya tukio alifika katika baa hiyo kwa lengo la kutaka kujua namna mauzo yanavyokwenda, lakini meneja huyo alimzuia kuingia kaunta na ndipo ilitokea kutoelewana na baadae ugomvi huo kutokea.

Kamanda Paulo alisema pamoja na maelezo hayo ya Cheka, lakini ameiagiza timu ya askari kuchunguza kwa kina tukio hilo ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment