Image
Image

Juhudi za kukomesha ndoa za utotoni za anza utekelezaji





Serikali ya Tanzania na washirika wake wa kimaendeleo wamesaini makubaliano mapya yenye lengo la kuongeza juhudi za kumaliza ukeketaji na ndoa za utotoni nchini humo.

Baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wa Tanzania Bibi Sophia Simba amesema serikali imedhamiria kutokomeza kabisa vitendo hivyo ili wasichana waweze kufurahia maisha yao bila ya kuwa na majuto katika maisha yao yote. Amesisitiza kuwa Tanzania itahakikisha kuwa hakutakuwa na wasichana watakaoolewa wakiwa na umri wa chini ya miaka 18, hususan baada ya katiba iliyopendekezwa kupitishwa. Tanzania ni moja ya nchi zenye kiwango kikubwa sana cha ndoa za utotoni duniani, karibu wasichana wawili kati ya watano wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment