Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya
ametoa wito kwa Jumuiya ya Afrika mashariki kuhimiza biashara ya ndani
ili kupunguza bidhaa zenye viwango vya chini kuingia katika kanda hiyo.
Akizungumza mjini Nairobi baada ya kukutana na maofisa wa shirikisho la vyama vya wajasiriamali wa sekta isiyo rasmi la Afrika mashariki, Rais Kenyatta amesema bidhaa za eneo hilo zinaweza kuifanya kanda hiyo kuwa eneo la kuzalisha bidhaa badala la kuagiza kutoka nje. Amesema inasikitisha kuona kanda hiyo inatunmia pesa nyingi kuagiza bidhaa zinazotengenezwa kwa malighafi wanayosafirisha nje.
Amesema serikali yake imeweka mipango ya kuwawezesha vijana na makundi mengine kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Maofisa wa jumuiya ya wajasiriamali wamependekeza kuwekwa kwa maduka katika sehemu ambazo wakazi wa nchi wanachama wanaweza kuonyesha na kuuza bidhaa zao kwa urahisi.
Akizungumza mjini Nairobi baada ya kukutana na maofisa wa shirikisho la vyama vya wajasiriamali wa sekta isiyo rasmi la Afrika mashariki, Rais Kenyatta amesema bidhaa za eneo hilo zinaweza kuifanya kanda hiyo kuwa eneo la kuzalisha bidhaa badala la kuagiza kutoka nje. Amesema inasikitisha kuona kanda hiyo inatunmia pesa nyingi kuagiza bidhaa zinazotengenezwa kwa malighafi wanayosafirisha nje.
Amesema serikali yake imeweka mipango ya kuwawezesha vijana na makundi mengine kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Maofisa wa jumuiya ya wajasiriamali wamependekeza kuwekwa kwa maduka katika sehemu ambazo wakazi wa nchi wanachama wanaweza kuonyesha na kuuza bidhaa zao kwa urahisi.
0 comments:
Post a Comment