Mbio hizo
zinashirikisha wakimbiaji mahiri kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Kenya,
moja ya nchi maarufu katika mchezo wa riadha Afrika na Dunia kwa ujumla.
Kukiwa hakuna mabadiliko makubwa ya njia zilizotumika mwaka jana,
washiriki watapita Barabara ya Mweka huku wakipata fursa ya kuuona Mlima
Kilimanjaro, ambao ndio mrefu kuliko yote Barani Afrika, ikiwa kama
sehemu ya kukuza utalii wa ndani pia.
Mbio zitaanza Chuo Cha Ushirika
mapema saa 12.30 asubuhi, huku kukiwa na mbio za full Marathon, half
marathon kwa wakimbiaji wa kawaida, half Marathon tena kwa watu wenye
ulemavu na Kilometa 5 kwa ajili ya afya.
0 comments:
Post a Comment