Image
Image

Naibu spika wa Bunge NDUGAI asisitiza umuhimu wa kufahamika kwa sheria ya manunuzi kwa wataalamu wa manunuzi

Naibu Spika wa Bunge JOB NDUGAI amesema fedha nyingi za serikali hutumika katika kufanya manunuzi mbali mbali katika sekta za umma na taasisi zake hivyo ni lazima sheria ya manunuzi ikafahamika vema kwa wataalamu wa manunuzi.
Akizungumza jijini ARUSHA, mara baada yakufungua kongamano la utawala bora katika ununuzi wa umma lililoshirikisha wakurugenzi na watendaji,wenyeviti na wajumbe wa bodi pamoja na Mameya na wenyeviti wa halmashauri nchini,ambaye amesema iwapo manunuzi yasipofanyika vizuri huweza kusababisha upotevu wa fedha pamoja na mianya ya rushwa.
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya udhibiti wa Ununuzi wa Umma nchini Balozi MATERN LUMBANGA,amesema
Changamoto kubwa inayowakabili ni uelewa mdogo kwa wahusika wa ,anunuzi kuhusu sheria ya manunuzi.
Baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema upo umuhimu wakupatiwa elimu kuhusu manunuzi ili kuepusha hasara yakupotea kwa fedha za umma nchini.
Wajumbe hao wa mkutano wa manunuzi ya umma wanakutana kwa siku TATU huku wengi wao wakitarajia kupata elimu kuhusu manunuzi sahihi ya umma.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment