Image
Image

Pistorius apandishwa hadhi gerezani kwa muda mfupi tu

Mwanariadha Oscar Pistorius ambaye anatumikia kifungo baada ya Mahakama ya Afrika Kusini kumkuta na hatia ya mauaji ya aliyekuwa mpenzi wake, Reeva Steenkamp kwa kumpiga risasi ndani ya nyumba yake sasa amepandishwa hadhi gerezani. 
Kwa mujibu wa utaratibu wa Magereza ya Afrika Kusini wafungwa wanapangwa kwa madaraja tofauti, Pistorious alikuwa 'Daraja B' lakini kwa sasa yuko 'Daraja A', ambapo hapa alipo sasa anaruhusiwa kukutana na wageni wowote wanaomtembelea mbali na ilivyokuwa mara ya kwanza alipotakiwa akutane na ndugu zake tu. 
Kwa sasa anaweza pia kusikiliza Radio, kuvaa vitu vya thamani kama cheni na pete. Msemaji wa familia yake Annalise Burgess amesema mwanariadha huyo kwa sasa amepandishwa hadhi na kuwa 'Daraja A', anaweza kupiga simu na kununua vyakula anavyotaka. 
Hata hivyo suala la Oscar kupandishwa daraja limewakera wafungwa wenzie walioko gereza la Death Island, ambao wamelalamika kuwa mwanariadha huyo anapewa hadhi hiyo ndani ya kipindi cha muda mfupi wakati wao wamekaa muda mrefu gerezani na hawajapata hadhi hiyo. 
Pistorius alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela mwaka jana mwezi August.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment