Image
Image

Polisi KIGOMA yasema vizuizi vilivyopo barabarani ni kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na kudhibiti usafirishaji wa vitu haramu


Kamanda wa polisi wa mkoa wa KIGOMA, JAFARI MOHAMED IBRAHIM amesema vituo na vizuizi vya polisi vilivyopo katika barabara kuu itokanayo mjini KIGOMA kwenda mikoa jirani vipo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi, kudhibiti usafirishaji wa vitu haramu, silaha na utoroshaji wa nyara za serikali na siyo kuwasumbua abiria.
Kamanda IBRAHIM ametoa kauli hiyo kufuatia kukamatwa kwa risasi 524, bunduki moja ya kivita aina ya SMG na Magazini zake tatu katika kizuizi cha POLISI kilichopo katika eneo la NDUTA wilayani KIBONDO zilizokuwa ndani ya HIACE iliyokuwa ikitokea KASULU kuelekea mjini KIBONDO.
Kufuatia kukamatwa kwa Risasi 524, bunduki moja na magazini tatu mkuu wa wilaya ya Kibondo Venance Mwamoto anayehamia wilayani KALIUA mkoani Tabora anasema suala ulinzi wa nchi Upo mikononi mwa raia wote
Halidhalika kamanda wa polisi wa mkoa wa Kigoma JAFARI IBRAHIM wakasema kuwa dhamira ya vizuizi vya polisi ni kudhibiti uhalifu na siyo kuwasumbua abiria ambao wakati mwingine wamekuwa wakilalamika unapofanyika upekuzi kwenye vyombo vya usafiri.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment