Image
Image

Serikali ya Kenya kupanua mpango wake wa kuboresha maeneo ya makazi duni

Serikali ya Kenya imetangaza kupanua mpango wake wa kuboresha makazi duni katika miji mingine ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha vijana kote nchini humo.
Msemaji wa ikulu Manoha Esipisu amesema, tangu mpango huo uanze Septemba mwaka jana, sehemu kubwa ya mtaa wa Kibera pamoja na makazi mengine mjini Nairobi zimesafishwa na barabara mpya kujengwa. Amesema kumekuwa na ongezeko la biashara kwa wafanya biashara wadogo na vijana wamefanikiwa kupata ajira.
Akizindua mpango huo mwaka jana, rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema miradi hiyo itaboresha mitaa duni ikiwemo Mukuru kwa Njenga, Korogosho na Mathare katika kaunti ya Nairobi. Ameongeza kuwa mpango huo unalenga kuwafanya wakazi wa maeneo hayo waishi katika mazingira safi yatakayowaepusha na vitendo vya uhalifu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment