Image
Image

Shekau: Tutavuruga uchaguzi mkuu wa Nigeria utakaofanyika mwezi ujao

Kundi la kigaidi la Boko Haram limetishia kuwa litavuruga uchaguzi mkuu wa Nigeria utakaofanyika mwezi ujao wa Machi. 
Abubakar Shekau, kiongozi wa kundi la Boko Haram nchini Ngeria ametoa vitisho kwamba kundi hilo litavuruga uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.
 Akizungumza kupitia mkanda wa video uliorushwa jana Shekau amesema kuwa Boko Haram haitaruhusu kufanyika uchaguzi mkuu huko Nigeria hata kama kundi hilo litalazimika kupoteza roho za wananchama wake. 
Uchaguzi mkuu wa Nigeria umepangwa kufanyika tarehe 28 mwezi ujao wa Machi. Uchaguzi mkuu nchini Nigeria awali ulipangwa kufanyika Februari 14, lakini uliakhirishwa kwa wiki sita nyingine kwa sababu za kiusalama, khususan kutokana na kushtadi mashambulizi ya Boko Haram kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.  
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment