Wakazi wa eneo la Mateka pamoja na Waendesha Bodaboda katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamelalamikia ubovu wa barabara ya Songea Girls hadi Mateka kwamba haipitiki wakati wa mvua na kusababisha ajali za mara kwa mara kutokana na ubovu.
Wamelalamikia ubovu wa barabara hiyo na kusema kero hiyo inashindwa kutatuliwa na sasa wamechoka na ahadi za kila siku za kuitengeneza barabara hiyo.
Wakazi hao wamewaomba viongozi wao kutowasahau kwa kuwa nao ni wakazi wa Manispaa ya Songea.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mateka, Manispaa ya Songea Bi. MARISTELA MAPUNDA amesema barabara hiyo iko katika mpango wa matengenezo ya kawaida.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment