Mashambulizi hayo yalifanywa dhidi ya ngome za kundi hilo zilizoko
nchini Libya siku moja baada ya kundi hilo kutoa video inayoonyesha
wakiwachinja raia 21 wa Misri ambao ni wakristo wa dhehebu la Coptic
nchini Libya.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la Misri imesema, mashambulizi hayo
yaliyolenga kambi za mazoezi pamoja na maghala ya silaha ya kundi hilo,
yalifanywa kwa kulipiza kisasi vitendo vya kigaidi ndani na nje ya
Misri.
Hii ni mara ya kwanza kwa Misri kuthibitisha hadharani kuwa
inafanya mashambulizi ya anga dhidi ya kundi hilo lililo nchi jirani ya
Libya.
Wakati huohuo jeshi la anga la Libya pia limesema kuwa limefanya
mashambulizi ya anga katika kambi moja ya kundi la IS mjini Darna,
mashariki mwa nchi hiyo.
0 comments:
Post a Comment