Wazalishaji na
wafanyabiashara wa sukari wakimsikiliza kwa makini maamuzi ya serikali
kuhusu bei ya sukari.
Waziri wa Kilimo
Chakula na Ushirika Mh. Stephen Wasira na Naibu wake (kushoto)
Mh.Godfrey Zambi, Bi. Sophia Kaduma Katibu Mkuu (kulia) na Dkt.Yamungu
Kayandabila (kushoto) wakifuatilia kwa makini mjadala baina yao na wazalishaji
na wafanyabiashara wa sukari katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Kilimo
Waziri wa Kilimo
Chakula na Ushirika Mh. Stephen Wasira akisisitiza jambo kwa umakini wakati alipokutana na wazalishaji
na wafanyabiashara wa sukari hapa nchini katika ukumbi wa mikutano hapa
wizarani .
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh.
Stephen Wasira akiendelea kuongea na wafanyabiashara wa sukari hapa
nchini.
Na.Mwandishi Wetu
Waziri wa Kilimo
Chakula na Ushirika Mhe Stephen Masatu Wasira amekutana na wadau wa sukari na
kutoa tamko la serikali kuhusiana na kupanda kwa ya sukari hapa nchini. Mhe
Wasira amewaagiza wazalishaji na wafanya biashara wa sukari hapa nchini
kuingiza sukari sokoni badala ya kuiweka kwenye maghala ili kushusha bei ya
bidhaa hiyo muhimu
Agizo hili la waziri limekuja
muda mfupi baada ya kupanda ghafla kwa bei ya sukari kutoka shilingi 1700/=
iliyokuwa ikiuzwa awali hadi shilingi 3000 kwa kilo.
Aidha hali hiyo ilisababishwa
na upungufu ulijiotokeza ghafla baada ya serikali kuthibiti uingizwaji holela
wa sukari toka nje ya nchi.
Upande wa Wadau wameahidi
kutoa ushirikiano kuhakikisha kuwa sukari inapatikana sokoni na kwa bei
nafuu.
Alisema Serikali kwa
kushirikiana na wadu wa sukari itaagiza tani 100000 ili kukabiliana na upungufu
unaotokea kila mwaka wakati viwanda vinapofungwa kwa ukarabati.
“Serikali itatoa kibali cha
kuingiza sukari tani 100000 mwezi machi ili kukabiliana na upungufu
utakaojitokeza pindi ukarabati” alifahamisha Mhe Wasira.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment