Image
Image

Waziri Nagu aitaka tume ya mipango kujielekeza katika kujibu changamoto za kiuchumi zinazo wakabili watanzania.



Waziri wa nchi (Ofisi ya Rais) Mahusiano na Uratibu, Mhe. Dkt. Mary Nagu amefanya ziara ya kujitambulisha kwa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ambayo ni moja taasisi anazoziratibu.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo Dkt. Nagu alitoa wito kwa Tume ya Mipango ijielekeze katika kujibu changamoto kuu za kiuchumi zinazowakabili watanzania kwa sasa ikiwemo umaskini miongoni kwa Watanzania walioko vijijini, ukosefu wa wa viwanda vya kuongeza thamani mazao hasa kipindi hiki Tanzania inapoelekea kwenye uchumi wa gesi.
Dkt. Nagu aliasa Tume ya Mipango kufanya tafiti mbalimbali za kiuchumi na kijamii zitakazotoa majibu ya changamoto hizo.
“Kwa kuwa moja ya majukumu ya Tume ya Mipango ni kuandaa mipango ya maendeleo ya muda mrefu, kati na ile ya kila mwaka na pia kufanya tafiti mbalimbali za kiuchumi na kijamii, napenda kusisitiza kuwa mipango inayoandaliwa ijielekeze katika kujibu changamoto hizo kubwa zinazowakabili wananchi wetu ili kuhakikisha kuwa tunafikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025,” alisema Dkt. Nagu.
Kwa mujibu wa malengo makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, serikali imejipanga kuhakikisha maisha bora na mazuri kwa kila mtanzania, utawala bora unaozingatia sheria, na kujenga uchumi imara, wa kisasa na ushindani.
Akizungumza wakati wa kumkaribisha Dkt. Nagu, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango alisema kuwa majukumu ya msingi ya Tume ya Mipango ni kutoa dira na mwongozo wa uchumi wa Taifa pamoja na kubuni sera za uchumi na mikakati ya mipango ya maendeleo ya Taifa; usimamizi wa uchumi na kufanya utafiti katika nyanja za uchumi na maendeleo ya jamii.
Dkt. Mpango aliongeza kuwa kwa sasa Tume ya Mipango inafanya kazi ya kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2014/15 pamoja na uandaaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2015/16 na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2016/17.
“Vilevile, Tume ya Mipango tumejidhatiti katika kuandaa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/17 – 2020/21 ambao utajikita katika kuifikisha tanzania kuwa ni nchi ya viwanda,” alisema Dkt. Mpango.
Kwa mujibu wa Dkt. Mpango, tangu kuundwa upya kwa Tume ya Mipango mwaka 2008, imefanikiwa kukamilisha kazi kubwa za kitaifa ikiwemo kufanya mapitio ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, kuandaa Mpango Elekezi wa Miaka 15 (2011/12 – 2025/26 pamoja na kuandaa Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/12 – 2015/16) na kuratibu utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Idadi ya Watu 2006.
Kazi nyingine ni pamoja na kuandaa Mipango ya Maendeleo ya Taifa kila Mwaka, kuandaa mfumo wa ufuatiliaji na utekelezaji wa miradi ya Matokeo Makubwa Sasa na kuratibu uanzishwaji wa President Delivery Bureau (PDB), Kuandaa Mwongozo wa Usimamizi wa Uwekezaji katika Sekta ya Umma (Public Investiment Management - Operational Manual – PIM-OM), na kufanya tafiti mbalimbali za kiuchumi na kijamii.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment