Image
Image

Idadi ya Waliofariki dunia katika ajali ya basi la Majinja Yafikia 40 huku wengine 23 Wakiwa wamehifadhiwa kwenye hospitali ya Mufindi Mkoani Iringa


Mkuu wa Mkoa wa iringa AMINA MASENZA amethibitisha Kuwa takribani watu 40 wamepoteza maisha na 23 wamejeruhiwa katika ajali iliyotokea mapema leo katika eneo la Changalawe mafinga mkoani humo baada ya basi la abiria  la Majinja  lenye namba za Usajili T438CDE  linalofanya safari zake kati ya Dar es salaam na mbeya kupata ajali baada ya kuangukiwa na kontena la lori la mizigo.
Amesema kuwa Maiti  zimehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mkoani iringa  pamoja na baadhi ya majeruhi ambapo majeruhi wawili ambao hali zao ni mbaya sana wamepelekwa katika hospitali ya rufaa ya iringa kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo.

Wanasema kuwa chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa basi hilo ambapo walimweleza Dereva Kupunguza mwendo lakini hakuweza kuelewa na hivyo katika mwendo kasi aliokuwa nao ndipo wakakutana na lori hilo na hatimaye kuvaana uso kwa uso baada ya juhudi za kulikwepa lori kufeli kutokana na barabara hiyo kuwa na mashimo yaliyoweza kufanya gari hilo kushindwa kukwepa mashimo hayo na hivyo kutokea kwa ajali.

Hata hivyo katika ajali hiyo imeelezwa kuwa wakati wakuwaokoa majeruhi na kutoa maiti wamekuta madaftari ya wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam ambapo inaelezwa kuwa katika gari hilo wanafunzi hao walikuwa ni wengi lakini bado haijafahamika kwamba walikodi gari hilo la Majinja ama la,lakini katika hospitali ya mufundi ndugu na jamaa wapo hospitalini hapo kwaajili yakuangalia ndugu zao na kutambua miili ya waliofariki dunia kufuatia ajali hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment