Kikosi cha ulinzi wa rais wa Marekani kinawachunguza maafisa wake wawili waandamizi kwa kuhusika na tukio la kugonga gari katika Ikulu ya Marekani.
Msemaji wa
Kikosi hicho, ameviambia vyombo vya habari tukio la ajali hiyo
lilitokea wakati wa jioni tarehe 4 mwezi huu.
Gazeti la The
Washington Post liliripoti kuwa maafisa hao waliendesha gari za
msafara wa usalama baada ya kukesha wakinywa pombe kwenye sherehe.
Tukio hilo la
ajali Ikulu ya Marekani, linaendeleza mlolongo wa matukio ya aibu
yaliyohusisha kikosi hicho chenye jukumu la kumlinda Rais Barack
Obama.
0 comments:
Post a Comment