Mdogo wa kiume wa msanii wa muziki Jose Chameleone,
Emmanuela Mayanja Hammertone maarufu zaidi kama AK47, amefrariki dunia usiku wa
jana baada ya kuanguka ghafla akiwa chooni katika pub maarufu ya Dejavu nchini
Uganda.
Mwili wa AK47 uligundulika majira ya saa 2 usiku na
kukimbizwa katika hospitali ya Nsambya na baadae kuthibitishwa kuwa tayari
amekwishapoteza maisha na zoezi la kuuaga mwili wa marehemu linafanyika leo
katika jengo la National Theater.
Salamu za rambirambi zimeendelea kumiminika kwa familia ya
Mayanja kufuatia taarifa za msiba huo mzito.
0 comments:
Post a Comment