Image
Image

Miili ya waliofariki Dunia katika ajali ya Majinja Mufindi Yaongezeka yafikia 43 huku 22 wakiwa wanapatiwa Matibabu zaidi.


Baadhi ya Majeruhi wa ajali hiyo wakiwa wamelala kitandani katika hospitali ya Mufindi iringa kwaajili ya kupatiwa matibabu kufuatia majeraha waliyoyapata kufuatia ajali hiyo.
Miili ya Watu waliofariki dunia jana kutokana na ajali ya Basi la abiria la Majijna Express lililokuwa na Namba za usajili T438 CDE lililokuwa limegongana na Lori la Mizigo lililokuwa limebeba Kontena ambalo liliangukia basi hilo na kuua watu 42 katika eneo la changarawe  barabara kuu ya Iringa na mbeya  hatimaye idadi imeongezeka na Kufikia Maiti 43 hadi sasa na majeruhi 26.

Kwa mujibu wa muandishi wetu anasema kuwa kinachoendelea muda huu ni zoezi la kuwatambua maiti waliofariki katika ajali hiyo katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa iringa na hospitali ya wilaya ya mufindi ambapo ndugu wa marehemu wameendelea kufurika hospitalini hapo kwalengo la  kuwatambua ndugu na jamaa zao.

Hata hivyo Taarifa iliyotolewa muda huu  na mganga mkuu wa mkoa wa iringa Dokta Robert Salim inaeleza  kuwa jumla ya maiti 26 wa ajali hiyo wamehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika  hospitali ya rufaa ya mkoa wa iringa na maiti wengine 17 wamehifadhiwa katika chumba cha maiti hospitali ya wilaya ya mufindi Mkoani Iringa

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa idadi ya kufikia maiti hao 43 hadi sasa ni kufuatia mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo aliyejulikana kwa jina la Oswald Mwinuka kufariki Dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa iringa na majeruhi wengine wawili wanangoja utaratibu wa rufaa ili kuwahamishia katika hospitali ya taifa ya rufaa ya muhimbili huku wengine wakiendelea na matibabu kwenye hospitali ya wilaya ya mufindi na hospitali ya rufaa ya mkoa wa iringa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment