Mjane wa Baba wa Taifa Mama MARIA NYERERE akukanusha Uvumi uliokuwa umeenea ndani na nje ya nchi kuwa Amefariki
dunia jana kupitia mitandao ya kijamii.
Akizungumza na Mwandishi wa kituo cha Runinga cha TBC Nyumbani kwake Msasani Jijini DSM
kufuatia uvumi huo, Mama MARIA NYERERE amesema alipokea simu kutoka kwa
Mmoja wa watoto wake aliyeko Butiama na kutaka kufahamu kuhusu hali yake
ya Afya baada ya kupata taarifa kupitia kwenye Mitandao ya Kijamii na
simu ya Mkononi kuwa Mama MARIA NYERERE Amefariki Dunia.
Aidha Mbali ya kukanusha uvumi huo, pia Mama MARIA NYERERE
amezungumzia kuhusu mauaji ya watu wenye ualbino yanayoendelea katika
sehemu mbalimbali ya nchi na kusema kuwa Watanzania hawana budi Kumlilia
mwenyezi Mungu ili aliepushe taifa na Balaa la Mauaji hayo
yanayoendelea kutokea nchini.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment