Mtangazaji wa kipindi cha Top Gear, Jeremy Clarkson yupo katika hati hati kuondoka BBC, baada ya kusimamishwa kazi kutokana na kuanzisha ugomvi wa kipuuzu na mmoja wa maprodyuza wa kipindi hicho.
Clarkson
anachunguzwa kwa kuanzisha ugomvi huo kwa kumpiga prodyuza Oisin
Tymon, kutokana na kupatiwa nyama baridi katika mlo wa usiku katika
moja ya hoteli ya kifahari.
Mtangazaji huyo
alikuwa anashinikiza kupewa pande la nyama baada ya kumaliza kupiga
picha za kipindi hicho, hata hivyo kwa wakati huo mpishi wa hoteli
hiyo alikuwa ameshaondoka.
Tayari mashabiki
wake 500,000 wametia saini mtandano kupinga Clarkson asifukuzwe, na
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron amesikika akisema anatarajia
tukio hilo halitamfukuzisha kazi mtangazaji huyo.
0 comments:
Post a Comment