Mt Number one naye ni
msani wa kizazi kipya na hadi sasa ameshatoa album mbili ambazo zote ziko
kwenye soko la kimataifa (international market) kama iTunes and Amazon na hata
ukitembelea YouTube zinapatikana.
Mt Number one alianza
muziki mwaka 2012 na hadi sasa ameendelea kufanya vyema hadi kufungua studio
yake.
“Lengo langu ni kufanya
muziki kwa kusapoti wenzangu pia nchi yangu ya Burundi na Afrika Mashariki kwa
ujumla .Ingawa niko Marekani kwa sasa ila nimeshajenga studio yangu huko
Burundi na pia nataka muziki wetu wa Afrika Mashariki ujulikane kila kona
duniani”. Amesema Mt Number one
Ukisikiliza muziki wake na
ukiangalia studio ambayo tayari ameiandaa utaelewa vizuri lengo la Mt Number
one la kuufikisha mbali muziki wa kizazi kipya. Bofya link hii kutazama moja ya
kazi yake https://www.youtube.com/watch?v=bBj1WQctVnw&app.
0 comments:
Post a Comment