Kupitia ukurasa wake wa Instgram Nay wa mitego siku mbili
zilizopita aliweka post ambayo ilikuwa inasema kuwa kwa sasa ana watoto watatu
na ana mapenzi ya kweli na watoto wake lakini hana mpango wala hana mahusiano
ya kimapenzi na mama wa watoto wake hao bali anawaheshimu wanawake hao kama
wazazi wenzake.
"Mr_Nay Baba wa watoto watatu... Sina Mke I mean
Sijaoa na sina mahusiano ya kimapenzi na Mwanamke yoyote Yule... Kati ya
niliozaa nao. Nawapenda watoto wangu nawaheshim mama zao..SingleBoy am in love
with my son and daughters... Rishma, Curtis na Munie"
Kwa upande wake Siwema ambaye ni mama wa Mtoto wa Nay juzi
aliweka picha ya Mzazi mwenzake na kuwataka mashabiki zake wafunguke lolote juu
ya picha ile ila Comment nyingi zilionesha kuwa watu hao hawapo sawa au hawapo
pamoja kwa sasa kama ambavyo baadhi zinasema.
"kaysamira: Siwema Mimi nakupenda siwez kukujudge
chochote sababu mapenzi upofu namuomba Mungu akupe jicho la tatu na uweze
kusonga mbele,mambo kama hayo hutokea na yanapita na kama yeye hakutaki usijali
kuna wanaume wengi tu wanaopenda kuwa na mtu kama wewe tena wazuri kuliko yeye
labda ndio chance mungu kawapa ili uweze kukutana na prince charm wako lakini
kama umeandikiwa kuwa na baba Curtis hakuna mwenye kupinga hilo lakini aache
kuwadhalilisha na kutumia udhaifu wenu kama mwanamke inauma anachezea sana
hisia zenu"
"Augustinasimon37: Hakuna wa kumjudge mtu hapa,
mapenzi ni ya wawili tu. kabla hakuzaa walikuwa sawa wakipendana iweje sasa
ndio maana tunaumia, tunawaombea wasiachane, kibinadam sio vizuri. Nakupenda
bure Siwema mpende mtoto wako ndio kila kitu kwako"
Lakini pia Nay wa Mitego leo amepost picha akitoka Mwanza
huku akiwa na Mwanae Curtis akimnywesha Maziwa ya kopo hali ambayo inaonyesha
wazi kuwa huenda mtoto huyo yupo chini ya himaya ya baba na si mama tena kitu
ambacho kinaweza kutoa majibu ya wazi kuwa watu hao huenda wameachana.
0 comments:
Post a Comment