Hata hivyo wanafunzi hao wameonekana wakililaumu jeshi la
zimamoto kwa kuchelewa kuja kuzima moto hali iliyowachuukua muda wanafunzi hao
kuzima moto huo wao wenyewe na hivyo gari la zimamoto lilivyofika kukuta tayari
moto huo umeshapunguza makali yake.
Kwa mujibu wa waziri Mkuu wa Serikali ya wanafunzi wa chuo
hicho cha UDSM Bwana Gibson George amesema kuwa chanzo hakijajulikana mara moja
juu ya kutokea kwa moto huo licha ya moto huo kusambaa maeneo mbalimbali ya
hosteli hizo.
" Watu wa zimamoto tumewapigia simu mapema sana ila wamechelewa kufika hadi muda
huu ndio wamefika,tumejaribu kuuzima moto na umepungua kidogo japo bado
unaendelea kwa baadhi ya vyumba" alisema Waziri Mkuu huyo.
0 comments:
Post a Comment