Image
Image

Watu ambao idadi yao haijafahamika mara moja wanaarifiwa kufariki dunia katika ajali iliyohusisha Lori na Basi la abiria Huko Changarawe Mafinga Mkoani Iringa.


Taarifa za awali kutoka eneo la tukio la changarawe mafinga mkoani iringa zinaeleza kuwa idadi ya watu ambao hawajafahamika  waliokuwa katika basi la majinja namba T438CDE linalofanya safari zake kati ya mbeya na Dar wamefariki dunia baada ya basi hilo kuangukiwa na kontena.

Hii ndio picha ikiwaonyesha Abiria wa Majinja wakiwa wamekandamizwa na Kontena hilo eneo la Mafinga Mkoani Iringa ilipo tokea ajali hii leo(Tunaomba radhi kwa Muonekano wa Picha usiokuwa wakuridhisha)


Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wanasema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni lori lilokuwa linakwepa mashimo ya barabra na kugongana na basi hilo la abiria uso kwa uso  ambapo  kamanda ya polisi mkoa wa iringa  RAMADHA MUNGI amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na amesema  atatoa taarifa kamili baadae
Licha ya kamanda kukiri kupata taarifa juu ya ajali hiyo taayari baadhi ya mitandao mbali mbali imekuwa ikiripoti kuwa watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni kati ya 40 hadi 50,kwa habari kamili tutawafahamisha itakapo toka taarifa rasmi juu ya waliojeruhiwa na kupoteza maisha kadri tunavyo endelea kufuatilia. 

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment