Image
Image

PINDA atembelea wahanga wa Mvua ya Mawe

Waziri Mkuu MIZENGO PINDA ametembelea baadhi ya familia zilizopoteza wapendwa wao pamoja na majeruhi waliolazwa kwenye hospitali ya wilaya ya KAHAMA kutokana na maafa ya mvua ya mawe iliyonyesha usiku wa
kuamkia jana.
Akizungumza na wafiwa katika vijiji vya MWAKATA na MAGUGUNG’HWA wilayani KAHAMA Waziri Mkuu amesema serikali haitawaacha katika kipindi hiki kigumu na kwamba serikali imepanga kupeleka vyakula, mahema, mablanketi na dawa ili kuwasaidia waathirika hao.
Waziri Mkuu PINDA ameagiza maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula - NFRA yaliyoko ISAKA kupokea misaada
ya chakula ili kuratibu misaada kwenda MWAKATA ambapo maafa yametokea.
Aidha taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu imesema serikali inapokea misaada mbalimbali kwa ajili waathirika na misaada hiyo inaweza kuwasilishwa Idara ya Kuratibu Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu DSM au kuwasilisha katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa SHINYANGA.
Zaidi ya watu 40 wamekufa na wengine zaidi ya 90 kujeruhiwa baada ya mvua ya mawe kunyesha Jumanne usiku katika kata ya MWAKATA wilaya ya KAHAMA mkoani SHINYANGA.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment