Image
Image

Ripoti yabaini uzembe uliofanyika katika utoaji misaada kupambana na Ebela umesababisha kuua zaidi ya watu 10,000




Dunia imelaumiwa kwa kushindwa kuitikia haraka kutoa msaada wa kupambana na mlipuko wa ugomjwa wa EBOLA uliotokea Afrika Magharibi na kuchangia kuenea haraka kwa ugonjwa huo na kuuawa zaidi ya watu 10,000 kufikia mwezi huu.

Katika ripoti ya kuadhimisha mwaka wa kwanza tangu kuzuka kwa mlipuko wa ugonjwa huo shirika la hisani la madaktari wasiokuwa na mipaka limesema taasisi nyingi zilishindwa kuchukua mkakati unaolenga athari ambazozingeepukwa.

Mwezi Januari mwaka huu kwenye mkutano wa dharura usio wa kawaida Shirika la Afya Duniani lilikiri kuchelewa kuitikia mlipuko huo na Mkurugenzi Mkuu wake DR. MARGARET CHAN anasema dunia pamoja na lishirika lake walikuwa goi goikuona kilichokuwa kinatokea mbele yao.

Katika miezi 12 iliyopita ugonjwa huo umeua watu 10,251 kwa mujibu wa ripoti ya shirika la afya duniani iliyotolewa tarehe 18 ya mwezi huu na wengi wao wakiwa Liberia zaidi ya 4000, Sierra Leone zaidi ya 3,700; Guinea zaidi ya 2,000 na Nigeria watu wanane.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment