Image
Image

Serikali imesema idadi ya Watanzania waliofungwa katika magereza nchini China ni 185 na kwmba Watanzania hao hawataweza kurejeshwa kutumikia vifungo vyao hapa nchini.


Serikali imesema idadi ya Watanzania  waliofungwa   katika magereza nchini China ni 185 na  kwmba   Watanzania hao hawataweza kurejeshwa kutumikia vifungo  vyao  hapa nchini.

Naibu Waziri wa  Mambo  ya  Ndani  ya Nchi,PEREIRA  AMME  SILIMA  ameliambia  Bunge  kuwa Tanzania haina mkataba na China wa kubadilishana wafungwa.

Amesema ni nchi mbili tu ambazo zilikuwa na mkataba na Tanzania ,   wa kubadilishana wafungwa ,   ambazo Thailand na Mauritius ,   ambazo hata hivyo mikataba hiyo imekwisha.

Naibu Waziri huyo wa  Mambo  ya  Ndani  ya Nchi   alikuwa akijibu swali la  Mbunge Viti Maalum ,  REBECCA MNGODO  aliyetaka kujua idadi ya  Watanzania  wanaotumikia vifungo nchini China  ]na uwezekano wa kurejeshwa kutumikia vifungo vyao hapa nyumbani.

Wakati huo huo, Serikali imewasilisha bungeni muswada wa sheria ya kudhibiti silaha wa mwaka 2014 ambapo kupitia muswada huo kutakuwa na ukomo wa kumiliki silaha pamoja na kutambuliwa silaha zinazotengenezwa kienyeji.
Akiwasilisha muswada huo Naibu Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Pereira Silima amesema kumekuwa na mapungufu makubwa katika umilikaji wa silaha hivyo kupitia muswada huo anatumai silaha zitamilikiwa katika utaratibu muafaka zaidi.
Kwa upande wake kaimu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya ulinzi na usalama Kapteni Mstaafu John Chiligati amesema moja kati ya mambo ambayo yatasaidia udhibiti wa umilikaji holela wa silaha ni wamiliki wote kutambulika bila kujali kama ni silaha zilizotengenezwa kienyeji au la.

Naye msemaji kambi ya upinzani katika kamati hiyo godbless lema amesema muswada huo siyo suluhu ya udhibiti matumizi holela ya silaha bali Serikali inatakiwa kutenda haki kwa wananchi wote kwani baadhi yao huzitumia silaha hizo katika kudai kile wanachodhani ni haki kwao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment