Image
Image

Serikali imesema kuwa inatambua mchango wa sekta binafsi katika Elimu

 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshugulikia Elimu, KASSIM MAJALIWA
Serikali imesema inatambua mchango wa sekta binafsi unaochangiwa katika elimu wenye lengo la kuboresha elimu nchini kwa kuweka miundombinu inayofaa.
Akizungumza wakati wa kukabidhiwa majengo ya Shule ya Msingi ya MAKTABA iliyopo UPANGA Jijini DSM Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshugulikia Elimu KASSIM MAJALIWA amesema michango kama hiyo inaunga mkono mikakati ya serikali ya maendeleo ya elimu ya msingi na sekondari pamoja na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa -BRN
Maktaba iliyopo imetolewa na Jumuiya ya Dini ya BAPS Charities ambapo mwenyekiti wa Jumuiya hiyo SUBHASH PATEL amesema jumuiya yao inaelewa umuhimu wa elimu hivyo itaendelea kushirikiana na serikali katika sekta ya elimu na kuwaomba wadau wengine wa elimu kujitokeza katika kuchangia kuboresha elimu nchini.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment