Serikali jijini Dar es Salaam imetoa
tahadhari kuhusu kuwepo kwa dalili za kufumuka kwa ugonjwa wa Dengue
katika kipindi hiki cha mvua, huku ikiwataka wananchi wanaoishi
mabondeni kuhama maeneo yao ili kunusuru maisha yao.
Akizangumza na waandishi wa habari leo ,
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Meck Sadiki amesema katika kuelekea
kwenye kipindi cha mvua mwezi huu magonjwa mengi hutokea kutoka na
kuongezeka kwa mazalia ya mbu na uchfunzi wa mazingira hivyo wananchi
wanatakiwa kujianda kwa lolote
“Hakuna mtu asiyetaka mvua, mvua ni neema na sasa
tunaelekea kwenye kipindi cha mvua, kipindi hiki huwa kinaambana
na milipuko mbalimbali ya magonjwa ukiwemo ugonjwa wa Dengue kwa
ajili ya maji kuhama na kutengeneza mazingira ya mbu, hivyo natoa
wito kwa wananchi kutunza mazingira yao.” Amesema Meck Sadiki
Meck Sadiki ameongezea kuwa mbu anayeendeza
ugonjwa huu hatari wa Dengue anapendakuishi na kuzaa kwenye maji
jaliyohifadhiwa kwenye ndoo, mapipa , tenki, vyungu vya maua na pindi
wanapozaliana kwa wingi husababisha maambukizi.
“Dalili za homa ya Dengue zinasababishwa na
virusi vinavyoambukizwa kupitia mbu huyu aina ya ‘aedes egptian’ na
husababisha homa kali, kuumwa kichwa , misuli na viungo mara kwa mara
pia mgonjwa huwa na kichefuchefu wakati wote.”amesema Meck Sadick
Ametoa wito kwa wananchi kusafisha mazingira ili
kuondoa mazalia ya mbu, na kutangaza kuwa utupaji wa taka ovyo ni
marufuku maana hizo taka zinachangia mitaro kuziba na maji kuhama, na
kuongeza kuwa watu wote wanatakiwa kuepuka mikusanyo isiyo ya lazima
ikiwa ni pamoja na kuvaa nguo ndefu.
Meck Sadiki amewataka wananchi kutumia vyandarua
vilivyo tiwa dawa na kuweka wavu na kuzuia mbu katika madirishani yao,
ikiwa ni pamoja na wale wananchi wanaoishi mabondeni kuhama haraka
maeneo yao kwani ni hatarishi Zaidi kwa mazalia ya mbu.
0 comments:
Post a Comment