Image
Image

Serikali yaunda kamati 2 kuchunguza ajali ya Mufindi

Serikali wilayani Mufindi imeunda Kamati mbili ikiwemo ya uangalizi wa mizigo ya abiria waliohusika kwenye ajali ya basi na lori iliyosababisha watu 50 kupoteza maisha Wilayani Mufindi mkoani IRINGA, huku miili AROBAINI na TISA iliyokuwa imehifadhiwa kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti katika hospitali za wilaya ya Mufindi na ile ya Rufaa tayari imetambuliwa .
Mkuu wa Wilaya hiyo MBONI MUHITA amesema Kamati hiyo itahakikisha kuwa mizigo ya abiria waliokuwa kwenye basi na ile ya kwenye lori inakuwa salama hadi ndugu wa marehemu watakapofika kuitambua.
Kabla ya Kuunda kamati hiyo, Mkuu huyo wa wilaya akiongozana na kamati ya Ulinzi na Usalama ikatembelea eneo la ajali na kutathmini chanzo cha ajali hiyo ili kuchukua tahadhari zaidi kwa siku za badae.
Mhita anasema kamati nyingine ya Kuchunguza chazo halisi cha ajali hiyo itatoa tathimini yake baada ya uc hunguzi.
Katika hatua nyingine Mganga Mkuu wa mkoa wa Iringa Dokta Robert Salim amesema kuwa miili 49 kati ya 50 iliyokuwa imehifadhiwa kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti katika hospitali za wilaya ya Mufindi na ile ya Rufaa ya Iringa imekwishatambuliwa na ndugu zao na kuchukuliwa kwenda kuzikwa.
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu Mwili mmoja uliobaki umetambuliwa kuwa ni wa raia wa Jamhuri ya Demokrasi ya Kongo ambaye unasubiri kuchukuliwa na ndugu zake.
Hali za majeruhi wa ajali hiyo zinaendelea vizuri huku wale waliolazwa Mufindi wakiruhusiwa wote huku majeruhi sita wakiendelea na matibabu hospitali ya Rufaa Iringa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment