Image
Image

Fupa la taya la binadamu wa kwanza lagunduliwa Ethiopia

Wanasayansi wamegundua taya wanaodai ni ile ya mtu wa kwanza duniani.
Kiolezo hicho chenye miaka millioni 2.8 kina miaka 400,000 zaidi ya ugunduzi wa utafiti unaosema kuwa mtu wa kwanza alitokeza.
Ugunduzi huo uliofanyika nchini Ethiopia unasema kwamba mabadiliko ya hali ya hewa yaliathiri maumbile ya binaadamu aliyetegemea miti hadi akaanza kutembea wima.
Mkuu wa kundi la utafiti amesema kwamba ugunduzi huo unatoa ufahamu wa kwanza kuhusu mabadilio muhimu ya binaadamu.
Proffessa Brian Villmoare kutoka chuo cha Nevada mjini Las Vegas amesema kuwa ugunduzi huo unatoa uhusiano kati ya binadaamu anayefanana na nyani kwa jina Lucy aliyeishi miaka millioni 3.2 ilioipita na ambaye aligunduliwa mwaka 1974 katika eneo hilo.
Je, Lucy aliyefanana na maumbile ya binaadamu ana uwezo kuwa alibadilika na kuwa binaadamu wa kawaida?
Lakini rekodi ya taya hiyo kati ya mda ambapo Lucy na nduguze waliishi na kutokea kwa mtu aliyekuwa na maumbile ya nyani aliyekuwa na ubongo mkubwa miaka millioni 2 iliopita imepishana kwa miaka mingi.
Taya hiyo ya chini ya mdomo ilio na miaka millioni 2.8 ilipatikana na mwanafunzi raia wa Ethiopia Chelachew Seyoun katika eneo la utafiti la Ledi-Geraru,katika jimbo la Afar.
Amesema kwamba alishangazwa alipokiona kifusi hicho.
''wakati nilipokipata kifusi hicho ,nilijua kwamba kina umuhimu mkubwa kwa kuwa huu ndio wakati unaowakilishwa na mabaki ya watu wa zamani mashariki mwa Afrika.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment