Rais wa serikali ya
wanafunzi UDOM akizungumza na Waandishi wa habari baada ya kuandamana hadi
nyumbani kwa Mh.Lowassa kumshinikiza kugombea urais mwaka huu.
Wanafunzi hao zaidi ya
300 walifika nyumbani kwake hapo majira ya saa sita mchana na kuzungumza nae na
kufikisha salamu zao ikiwa ni pamoja na kumchangia fedha za kuchukulia fomu.
Aidha Lowassa kwa Upande
wake amewashukuru vijana hao na kusema kuwa ujio wao na ule wa masheikhe wa
Bagamoyo unazidi kumhamasisha kutangaza nia na pindi muda ukifika anaweza
kufanya hivyo.
Mbunge wa Monduli na
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiwasalimia mamia ya wanafunzi wa vyuo vya
elimu ya juu mkoa wa Dodoma, waendesha boda boda na wamachinga wa mkoa huo
walioandamana hii leo hadi nyumbani kwake Area D mjini Dodoma kumuomba pindi
wakati ukifika kwa mujibu wa taratibu za chama cha Mapinduzi (CCM) asisite
kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais.
Lowassa amesema anazidi kuhamasika kufuatia maombi ya watu wa makundi mbalimbali ya jamii wanao muomba kugombea urais mwaka huu. Aidha na yeye amewaomba vijana hao na makundi mengine kuwahimiza wenzao vyuoni na hata mitaani kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ili siku ya uchaguzi wawe na sifa za kuweza kushiriki katika uchaguzi kwa kupiga kura.
Lowassa amesema anazidi kuhamasika kufuatia maombi ya watu wa makundi mbalimbali ya jamii wanao muomba kugombea urais mwaka huu. Aidha na yeye amewaomba vijana hao na makundi mengine kuwahimiza wenzao vyuoni na hata mitaani kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ili siku ya uchaguzi wawe na sifa za kuweza kushiriki katika uchaguzi kwa kupiga kura.
0 comments:
Post a Comment