Akisomewa
mashtaka wawili yanayomkabili na mawakili waandamizi wa serikali kwa upande wa jamuhuri ambao ni shadrack kimaro
na tumaini kweka, mbele hakimu wilfred dyansobera,wamesema askofu josephat
gwajima alitenda kosa la kwanza la kutoa lugha ya matusi akiwa katika viwanja
vya tanganyika peakers kawe jijini dar es salaam dhidi askofu mkuu wa kanisala
katoliki cardinary pengo huko kosa la pili ikiwa ni kushindwa kuhifadhi silaha
pamoja na risasi wakati akiwa katika hospitali ya tmj jijini Dar es salaam
kinyume na sheria za silaha za moto.
Baada
ya hakimu mh wilfred dyansobera kusikiliza pande zote ikiwemo upande wa jamhuri
na upande wa mlalamikiwa,katika makosa yote mawili, baada ya wakili wa askofu
gwajima Dr.PeterKibatala kuoomba mahakama kumuachia mteja wake kwa
dhamana,mahakama iliridhia na kumuachia huru askofu Gwajima kwa dhamana ambapo
katika kosa la kwanza amejidhamini mwenyewe kwa kutoa shilingi milioni moja na
katika kosa ya pili ametolewa na dhamana ambapo baada ya mahaka kumuachia huru
pamoja na baadhi ya wafuasi wake watatu
walikamatwa na kufikishwa mahakamani hapo.
Kabla
ya hapo ITV ilishuhudia askari wa jeshi la polisi wakiwa wamezingira geti la
askofi Gwajima nyumbani kwake salasala hali iliyotia hofu kwa wakazi wa maeneo
hayo na viongozi wa maeneo hayo kama anavyoeleza mwenyekiti wa serikali ya mtaa
wa kilimahewa kata ya wazo alipojengwa askofu Gwajima.
Baada
ya askari wa jeshi la polisi kuondoa katika nyumba ya skofu Gwajima ,umati ya
waumini wake walimiminika nyumbani kwake ambapo baada ya muda mfupi alioondoka
kwenda katika kituo kikuu cha polisi CENTRAL ambapo baada ya kuingia ndani na
kukaa kama dakika 10 aliondolewa chini ya ulinzi na kufikishwa katika mahakama
ya hakimu kisutu.
Baada
ya kuachiwa huru waumini wake waliofika mahakamani hapo walianza kuimba nyimbo
ambapo kwa mujibu wa wakili wa askafu Gwajima anatakiwa kupanda kizimbani tena
tarehe 4 mwezi may 2015 akiongozana na wafuasi wake walioshtakiwa.
Chanzo ITV
0 comments:
Post a Comment