Image
Image

Balozi wa Malawi nchini kuzikutanisha taasisi za sekta binafsi za Tanzania na Malawi katika Nyanja ya uwekezaji.


Balozi wa Malawi nchini  Mhe.  Hawa Ndilowe amesema yupo tayari kuzikutanisha Taasisi za sekta binafsi  za Tanzania na Malawi ili zijadili uwekezaji wa biashara kwa njia ya ubia kwa faida ya pande zote mbili.
Balozi wa Malawi nchini Mhe. Hawa  Ndilowe ameyasema hayo jijini Dar es salaam alipomtembelea ofisini kwake Mwenyekiti wa Sekta Binafsi nchini – TPSF Dr. Reginald Mengi.

Kauli ya Balozi huyo inatokana na ushauri wa  Dr. Mengi kuwa Wafanyabiashara wa Tanzania na Malawi hawana budi kushirikiana katika biashara za ubia ili kujiimarisha kiuchumi   na kudumisha ujirani mwema, na kusisitiza kuwa ili uwe endelevu, ushirikiano huo ujadiliwe katika ngazi ya uongozi wa Taasisi za sekta binafsi:…

Dr. Mengi pia amezishauri nchi za Afrika kufanya biashara baina yao kwa kuacha kasumba ya  kupenda kuagiza bidhaa kutoka nje ya bara hili.

Pia amezishauri nchi za Afrika kuwawezesha wananchi wake kudhibiti na kumiliki uchumi wa nchi ili kudumisha amani na utulivu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment