Jeshi la polisi mkoani Morogoro
limewakamata watu tisa wakiwa na silaha za kulipua
na nguo za jeshi la wananchi wakiwa wamejifungia katika msikiti wa
Suni Kidatu wilayani kilombero mkoani
Morogoro.
Kamanda wa polisi mkoa
wa Morogoro lenard Paul amesema tukio la kukamatwa kwa watu hao limekuja
kufuatia jeshi la polisi kupata taarifa za uhalifu ambapo jambazi
mmoja aliruka katika bajaji na kisha kumjeruhi askari shingoni ambapo wananchi
wenye hasira kali walioshuhudia tukio hilo
walimkimbiza jambazi huyo akiwa na silaha na kisha kumchoma
moto.
Kamanda Paul amesema
kufuatia tukio hilo jeshi la polisi liliongeza nguvu ya askari
ambapo walifanya msako mkali na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine wakiwa
katika msikiti wa Suni Kidatu na baada ya kupekuliwa wamekutwa na vifaa vya
Milipuko,Nguo za jeshi la wananchi (JWTZ) ambapo jeshi hilo linaendelea kuwashikilia
watuhumiwa na kunataarifa kuwa watuhumiwa hao walijiandaa kufanya
tukio la uhalifu.
Aidha kamanda Paul
amewashukuru wananchi wa Ruhembe Kidatu wilayani kilomeroa mbao wametoa
ushikiano kufanikisha kukamtwa kwa watuhumiwa hao.
0 comments:
Post a Comment