Image
Image

Breaking News: Wimbi la ajali laendelea kuwatesa wasafiri,19 wafa kwa ajali ya Hiace wilayani Rungwe Mkoani Mbeya





Watu 19 wamefariki dunia baada ya Hiace waliokuwa wakisafiria kuacha njia na kupinduka maeneo ya Kiwira wilayani Rungwe Mkoani Mbeya.
Miili ya watu kumi na tisa waliofariki dunia ikiwa inaonekana imelazwa chini hapo huku ndugu jamaa na mashuhuda wakiangalia namna hali ilivyokuwa.


Watu 19 kati yao 17 wamefariki dunia  papo hapo na wengine watatu wamejeruhiwa baada ya gari dogo la kusafirisha abiria aina ya toyota Hiace kushindwa kukata kona kali katika eneo la Kiwira wilayani Rungwe na kupinduka kabla ya  kutumbukia mtoni.
Gari hilo lenye namba za usaji T290 ABU ambalo limesajiliwa kufanya safari zake kama daladala jijini mbeya, leo asubuhi limepakia abiria wapatao 20 kwa ajili kuwasafirisha kwenda tukuyu wilani Rungwe na likiwa katika mwendo mkali dereva wake ameshindwa kukata kona kali za ilongobota, eneo lijulikanalo maarufu kwa jina la uwanja wa ndege na kutumbukia katika mto kiwira kama ambavyo baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wanavyoeleza.
Kaimu mganga mkuu wa wilaya rungwe Dk. Aminiel Ngumuo amekiri kupokea miili 17 ambayo imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Rungwe,makandana na majeruhi watatu ambao  wanatibiwa katika hospitali ya misheni ya igogwe ambako pia mwili majeruhi aliyefariki wakati akipelekwa hospitalini hapo umehifadhiwa.
Kamanda wa polisi mkoa wa mbeya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo chake ni mwendo kasi, huku akiwata madereva kuwa makini barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment