Image
Image

CHADEMA:Hatuwezi kukubali serikali ya awamu ya nne kuongezewa muda kuongoza nchi kutokana na mchakato wa zoezi la daftari la wapiga kura kusuasua.



Chama cha demokrasia na maendeleo -CHADEMA- kimesema hakitakubali serikali ya awamu ya nne kuongezewa muda wa kukaa madarakani kutokana na kusuasua kwa zoezi la uandikishwa wa daftari la wapiga kura.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa chama hicho wa ngazi ya shina hadi wilaya wa mkoa wa Dar es salaam, mwenyekiti wa Chadema taifa ameitaka serikali kuharakisha zoezi la uandikishaji wapiga kura na kusisitiza tarehe ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ilijulikana nchi nzima kutokana kuwepo kikatiba na kisheria kuwa ni jumapili ya mwisho wa mwezi wa 10.
Awali wakizungumza na mamia ya viongzoi wa chama hicho katika mkutano huo naibu katibu mkuu wa chadema Zanzibar Bwana Salum Mwalimu amesema lengo la chama hicho kuwa na viongozi wenye weledi na uwezo wa kufanya kazi,huku  naibu katibu mkuu wa chama hicho Tanzania bara Mhe. John Mnyika amesema mafunzo hayo yataendeshwa nchi nzima ambapo yanatarajiwa kuwafikia viongozi wa chama zaidi ya laki 2 na ishirini na nne elfu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment