Chama cha demokrasia na maendeleo -CHADEMA- kimesema hakitakubali serikali ya awamu ya nne kuongezewa muda wa kukaa madarakani kutokana na kusuasua kwa zoezi la uandikishwa wa daftari la wapiga kura.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa
mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa chama hicho wa ngazi ya shina hadi wilaya
wa mkoa wa Dar es salaam, mwenyekiti wa Chadema taifa ameitaka serikali
kuharakisha zoezi la uandikishaji wapiga kura na kusisitiza tarehe ya kupiga
kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ilijulikana nchi nzima kutokana kuwepo
kikatiba na kisheria kuwa ni jumapili ya mwisho wa mwezi wa 10.
Awali wakizungumza na mamia ya
viongzoi wa chama hicho katika mkutano huo naibu katibu mkuu wa chadema
Zanzibar Bwana Salum Mwalimu amesema lengo la chama hicho kuwa na viongozi
wenye weledi na uwezo wa kufanya kazi,huku
naibu katibu mkuu wa chama hicho Tanzania bara Mhe. John Mnyika amesema
mafunzo hayo yataendeshwa nchi nzima ambapo yanatarajiwa kuwafikia viongozi wa
chama zaidi ya laki 2 na ishirini na nne elfu.
0 comments:
Post a Comment