Image
Image

News Alert: Chakuwa yashangazwa na kitendo cha SUMATRA kushindwa kukokotoa na kushusha nauli za daladala.


Chama cha kutetea abiria nchini chakua kimeeleza kushangazwa na kutoridhika na kitendo cha  mamlaka ya uthibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA kushindwa kushusha nauli kwa abiria wanaotegemea usafiri wa daladala kila siku na kueleza kuwa hatua hiyo ni kuwakandamiza wananchi wa kipato cha chini.
Hayo yamebainishwa na katibu wa chama cha kutetea abiria chakua Bwana Godwin Mtongeji jijini dar es salaam na kueleza kuwa sababu zilizotolewa na SUMATRA za kushindwa kushusha nauli kwa kigezo cha usumbufu wa chenji haina mashiko na imeangalia upande mmoja wa wamiliki wa daladala huku wakieleza kushangazwa na nauli za mikoani kushuka kwa kiwango kidogo sana ambapo kwa baadhi ya ruti za mikoani unakuta tofauti ya nauli za sasa na zazamani ni kati ya 1800 mpaka 3000.
TAMBARARE HALISI ilipata nafasi ya kupita katika baadhi ya  vituo mbali mbali vya daladala jijini dar es salaam kusikia nini maoni ya wakazi wa jiji hilo juu ya swala hili la nauli?. ambao baadhi yao wameeleza kutotendewa haki na SUMATRA kutokana na kutoshuka kwa nauli hizo jambo linalowapa wasiwasi wa uwepo wa maslahi binafsi katika kuamua maswala haya ya kushusha nauli na kusababisha kutowatetea wananchi wa hali ya chini ambao ndiyo wanaotakiwa kuangaliwa sana.
Wamesema ipo haja yakuona kuwa wananchi kipato wanachokipata nikidogo mno ambapo hali ya uchumi nayo inaonekana kuyumba hivyo ingekuwa jambo la busara kwa SUMATRA kuona kunahaja ya ushushaji wa nauli kwa dala dala jijini na ikizingatiwa kwa upande wa vijana hali si shwari kwakuwa hawana kazi za kuaminika za kuwaingizia kipato licha ya pesa wanayoipata hutumika nauli na kula jambo ambalo linawafanya kusonga mbele kiuchumi.
Nisiku ya pilio leo tangu mamlaka  ya uthibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA kutangaza  viwango vipya ya nauli vitakavyoanza kutumika april 30 mwaka huu ambapo nauli za mabasi ya mikoani ndizo zilizoshushwa kwa asilimia 7.8 na kuziacha nauli za daladala zikiwa zilezile kwa madai kuwa katika ukokotoaji ili kushusha nauli za dala dala imeshindikana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment