Ghala
hilo lililopo eneo la ilemela jijini mwanza limekutwa likiwa limesheheni zaidi
ya 120 za dawa ambazo ni sawa na tani 42 zikiwemo dawa za serikali za Kenya na
Uganda, dawa za misaada, dawa zilizopigwa marufuku nchini kama vile klorokwini
ya sindano, amodiaquine na gripe water -dawa nyingine zilizokutwa ndani ya
ghala hilo na kwenye duka lake la dawa lililopo Natta barabara ya nyerere ni
pamoja na ambazo hazijasajiliwa na TFDA na azisizoruhusiwa kuuzwa kwenye maduka
ya dawa.
Meneja
wa usalama wa dawa wa TFDA Kissa Mwamwitwa ndiye aliyeongoza zoezi hilo
liliendeshwa chini ya usimamizi mkali wa askari polisi wenye silaha za moto.
Baadhi
ya maofisa wanaotekeleza operesheni hiyo, wakiwemo wanasheria kutoka TFDA na
baraza la famasi tanzania pamoja na meneja wa mamlaka hiyo kanda ya kati
Florent Kyombo wakizungumzia tukio hilo wamesema taratibu za kisheria
zinafanyika ili kumfikisha mahakamani mtuhumiwa.
Mwenyekiti
wa serikali ya mtaa wa kahasa ilemela Richard Peter alikuwa shuhuda wakati
maofisa hao wa TFDA, baraza la famasi tanzania na askari polisi walipokuwa
wakitekeleza zoezi hilo kwenye ghala la dawa ambalo linasemekana bado
halijasajiliwa na TFDA huku mmliki wake charles mbusiro akitoroka
kwa kuruka ukuta na kutokomea kusikojulikana.
0 comments:
Post a Comment