Image
Image

Gwajima:Siogopi mtu wala kufa


ASKOFU wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima,amesema haogopi mtu yeyote wala kufa bali ataendelea kuinyoosha nchi anapoona haiendi sawa.
Alitoa kauli hiyo Dar es Salaam jana,wakati wa mahubiri yaliyofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers Kawe.
Alisema uhusiano wake na watu mbalimbali wakiwamo wanasiasa utaendelea kubaki palepele.
Kwa mujibu Askofu Gwajima, baadhi ya watu wamekuwa wakimhusisha kuwa na urafiki na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa jambo ambalo alikiri ni la ukweli kwa sababu walifahamiana tangu mwaka 1996.
“Niliwahi kumuita Waziri Mkuu Mizengo Pinda mara nne hapa ili aje azindue moja ya kazi zangu,hakuja badala yake nilimuita Lowassa na aliitikia wito wangu na kuja kuifanya kazi hiyo hivyo siwezi kumuacha.
“Wapo viongozi wengi ambao wanakuja kusali katika kanisa langu, kwa mfano Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM,Nape Nnauye, kwa nini wasimseme yeye badala yake wanamsema Lowasa tu?.
“Nashangaa mnatoka mlipotoka mnaongea kwa kubana pua, ukimuogopa mtu nchi itakuwa haiendi vizuri na mimi sitaogopa kukemea mambo ambayo hayafai katika jamii, mfano suala la Escrow.
“Nitaendelea kuinyoosha nchi ninapoona haiendi sawa.
“Siwezi kwenda mbali na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Willbrod Slaa hata kama atakuwa Rais… na yeye pia ni rafiki yangu,” alisema Askofu Gwajima.
Katika ibada hiyo aliliombea Taifa amani, uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu na kikao kijacho cha Bunge la Bajeti linalotarajia kuanzia baadaye mwezi ujao.
Wiki iliyopita, Askofu Gwajima alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mashitaka mawili ambayo ni kumtolea lugha ya matusi ambayo imemfedhehesha Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, na kuweka vibaya silaha anayomiliki.
Source:Mtanzania
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment