Image
Image

Hospitali ya taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam imezindua huduma yake ya kuzibua mishipa ya moyo iliyoziba kwa wagonjwa waliokuwa wakisafirishwa nje ya nchi kupatiwa huduma hiyo.


Kwa mara ya kwanza katika historia ya tanzania hospitali ya taifa muhimbili imezindua huduma ya kuzibua mishipa ya moyo iliyoziba baada ya kupata kifaa maalum  cha kazi hiyo  ambapo kitasaidai wenye matatizo hayo ambao walilazimika kusafrishwa nje kupata huduma hiyo.
Hayo yamebainika na mkuu wa kitengo cha upasuaji wa moyo Dk. Evarest Nyawawa wakati wa ufunguzi wa mashine ya ya uchunguzi wa mishipa ya moyo na kuzibua mishipa ya iliyoziba kwenye moyo na kuweka kifaa maluum kiitwacho STENT ili kuruhusu damu kuendelea kusukumwa ambapo amesema kwa wagonjwa wa mijini maradhi hayo yanatokana na ukosefu wa mazoezi na ulaji mbaya usiozingatia lishe bora.
Kwa upande wake mkuu wa idara ya tiba na upasuaji moyo Prof. Mohamed Janabi amesema dhana ya kuongeza ushirikiano na nchi nyingine ni kuboresha huduma za upasuaji wa moyo ambapo kutokana na kuwepo na kifaa hicho sasa muhimbili kupitia kitengo cha moyo inaweza kupokea wagonjwa kutoka jumuiya ya afrika mashariki nakuongeza kuwa kwa kipindi cha mwaka mmoja wameweza kuwafanyia upasuaji wa moyo wagonjwa.
Mmoja wa madaktari kutoka india ambaye anashirikiana na madaktari kutoka marekani ambao wameletwa na  serikali kufanya upasuaji huo na kuwafundisha madakatari wa hapa nyumbani ameeleza tatizo hilo linawakumba sana nchi zinazoendelea huku daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa hospitali ya muhimbili akieleza kuwa mashine hiyo itaokoa gharama kubwa serikali iliyokuwa inatumia kupeleka wagonjwa nje ya nchi ambapo mgonjwa mmoja wakati mwingine alikuwa anatumia zaidi ya milioni 20.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment