Baadhi ya makada wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Arusha wamesema usaliti , majungu na unafiki unaoendelea ndani ya chama hicho visipodhibitiwa ,chama hicho kitaendelea kushindwa katika chaguzi zinazotarajiwa kufanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo .
Wakizungumza wakati
wa kumsimika Kamanda wa vijana wa Kata
ya Sombetini , Bwana BAKARI
MSANGI ,makada hao wamesema
inasikitisha kuona hata
viongozi wa juu wanawajua
watu wanaokisaliti chama ,lakini
hawachukui hatua badala yake
wanabaki kulalamika .
Akizungumzia malalamiko hayo Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi wa
Wilaya ya Arusha,Bwana WILFRED SOILELI ,pamoja na kukiri
kuwepo kwa makundi
yanayotajwa kuwa yanakihujumu
chama , amewataka watajwe
hadharani ili wachukuliwe
hatua .
Kwa upande
wake kamanda wa vijana aliyesimikwa
Bwana BAKARI RAHIBU MSANGI
amewa taka vijana kuwa wa
kwanza kupambana na watu
wanaokisaliti chama na
kutowafumbia macho baadhi ya watu wanaofanya vitendo
hivyo .
0 comments:
Post a Comment