Wananchi wa jijila Arusha wakiwemo
wanaoendesha shughuli zao katika masoko likiwemo la kilombero wako
hatarini kukumbwa na magonjwa ya milipuko kutokana na kukithiri kwa
uchafu unaotokana na kutowajibika kwa watendaji wenye dhamana ya kusimamia
usafi
Baadhi ya wanachi wanaokabiliwa na tishio hilo wakiwemo mama lishe wamemweleza mkuu wa wilaya ya arusha Bw. Christopher Kangoe kuwa wanapowauliza watendaji wa sekta ya afya juu ya tatizo hilo wawajibu kuwa serikali haina fedha.
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Bw.Juma Iddy amesema ameshapokea malalamiko ya tuhuma za watendaji hao na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa dhidi yao sambamba na kushughulikia tatizo la msingi.
Akizungumza na watendaji wote wa wilaya ya arusha mkuu wa wilaya Bw.Christopher Kaangoye amesema kama kuna mtendaji anayedhani kuwa hawezi kutimiza wajibu wake ni bora akaondoka kwani hali iliyopo haivumiliki.
Baadhi ya wanachi wanaokabiliwa na tishio hilo wakiwemo mama lishe wamemweleza mkuu wa wilaya ya arusha Bw. Christopher Kangoe kuwa wanapowauliza watendaji wa sekta ya afya juu ya tatizo hilo wawajibu kuwa serikali haina fedha.
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Bw.Juma Iddy amesema ameshapokea malalamiko ya tuhuma za watendaji hao na kwamba hatua zinaendelea kuchukuliwa dhidi yao sambamba na kushughulikia tatizo la msingi.
Akizungumza na watendaji wote wa wilaya ya arusha mkuu wa wilaya Bw.Christopher Kaangoye amesema kama kuna mtendaji anayedhani kuwa hawezi kutimiza wajibu wake ni bora akaondoka kwani hali iliyopo haivumiliki.
0 comments:
Post a Comment